MATANGAZ0 YETU 



Breaking

Monday 6 March 2017

CHOMBEZO LA HUBAA

alfachengula.blogspot.com"CHOMBEZO"

*UTAMU WA MCHEZO*

Mtunzi: michael mejah.
Mahali: masaki.
Namba: 0655085519.

EPISODE ONE.
"wewe clementina ebu amka uendi chuo wewe?"

"mama jamani naumwa"

"mtoto mvivu wewe unaumwa unaumwa nini unaona shida kuamka ebu amka usaidie kazi uende chuo"

"aah mama naamka lakini mama nilikwambia mwambie dadie alete mfanyakazi ila mbishi ona kazi zote unafanya peke yake"

"una wazimu wewe upo mimi pia mfanyakazi tuna mtoto wa kulea ebu nitolee ujinga wako yani wewe huku utakapoolewa utawapa shida tu"

"mmh mama tuyaashe naona unaenda mbali"

"ndo uamke hapo"

Nilijivuta kutoka kitandani nikachukua kanga yangu na kujifunga kiunoni kisha blauzi yangu nikaingia jikoni kucheki ustarahabu nikagundua mambo yote sawa nikarudi zangu chumbani angalau nikajisafishe huu mwili. "ooh mungu wangu saa tatu na robo! Aki ya mama hizi movie na internet vitaniua kila nikijitahdi kuwahi kulala saa tisa, nane, kumi ndo mida yangu" nilijikuta naropoka baada ya kuangalia simu yangu, hapo chuo saa nne kipindi cha kwanza CBE.

"mamie see later am just go to the collage/mama tutaonana baadae naenda chuo" nilimuaga mama baada ya kumaliza kunywa chai.

"okey baadae"

Nilichukua toyota VX ya mama nikaenda nayo chuo kwani mama hakuwa na safari siku hiyo. Mara zote huwa naenjoy nikiwa na this car more than nikitumia gari yangu spacio, basi hapo nitasikiliza mizika mpaka chuo na nyimbo ninazozirudia mara nyingi ni nicki minaj-night a still young, wizkid-ojuelegba, daimond-ukimuona, burna boy-soke na zahara-destiny. Nazipenda sana hizi nyimbo.

"eeh vipi clementina unachange magari daily mtoto wa kisure sana wewe"

"aah jèff wa kisure mimi au wewe unayetumia mitablet ya nguvu"

"aha wewe ya kichina tu hii usipagawe sana"

" acha kuzingua wewe, oya vipi paul yupo? Maana sikuwa na mpango wa kuja chuo but nimekuja kwa ajiri yake"

"yani cleme you don't care umechelewa kipindi, paul ameenda kivukoni mara moja na kule kwenu lecture kisha ingia nusu saa zilizopita"

"ahaa lecture gani huyo?

"si hon. Msingwa"

"mzinguaji yule stori nyingi ngoja nisubiri kipindi cha junior yule ndo namkubali"

"poa bwana mida me naenda zangu classroom profesa rwemamu anaingia muda si mrefu"

Nilibaki nimekaa pale nachat mara whatsaap, instra, fb, imo na wechat ili mradi tu muda uende ama aje paul au niingie kipindi cha pili. Paul ni mpenzi wangu miezi sita sasa yeye yupo stashahada pale mimi nipo diploma in business adiministration.
**:-*

Baada ya kumsisitiza sana dadie amlète dada wa kazi maombi yalijibiwa siku hiyo nikiwa na kaka clement na dogo langu clinfford baba alikuja na mfanyakazi mdada wa kinyeramba mweupe ana shepu tu utasema si mfanyakazi labda mtoto wa ndani pale. Wote tulifurahi ujio wake ila mama hakupenda na hata chakula siku hiyo akula kwa ghaziba iliyomjaa.

Mida ya saa sita hivi nilipomaliza kuangalia movie ya series ya the marine nilikuwa koridoni kuelekea chumbani nikasikia sauti kutoka chumbani kwa baba na mama hisia zikanipanda..

JE NI SAUTI GANI HIZO. Usikose kufatilia chombezo ili la clementina.

No comments:

Post a Comment