MATANGAZ0 YETU 



Breaking

Sunday 11 June 2017

TUNDU LISSU:RAISI AKIFANYA YAFUATAYO NITAKUA TAYARI KUUKUBALI UTEUZI WAKE

Raisi wa chama cha wanasheria nchini na Mbunge wa Singida Mashariki Muheshmiwa TUNDU Lissu amesema atakapoteuliwa na raisi hatokubali mpaka pale atakafanya yafuatayo wakati akihojiwaa
Swali: Labda itokee Mh. Rais amekuteua kwenye nafasi yoyote ile ambayo ana mamlaka nayo, itakuwaje?
Lissu: Kwanza nikutoe wasiwasi haitatokea,Pili, hata ikitokea Rais akafanya hivyo, nitamwambia mheshimiwa mimi napinga mfumo uliokuweka madarakani. Tunataka Katiba mpya, tunataka tutengeneze nchi upya. Kwahiyo kwanza hawezi na pili akinijaribu nitamwambia wazi kwamba kama unataka niitumikie nchi hii tubadilishe Katiba na tuiweke nchi sawa kwenye misingi sawa. Lakini mimi siwezi kutumikia utawala wa kidikteta kwa nafasi yoyote ile. Mimi ni mpinzani, na ndio maana nipo Mahakamani kila siku. Wanaopewa hizo nafasi sio wapinzani, ni watu wanaotumiwa kuua upinzani na hawataweza.

No comments:

Post a Comment