serikali imeviagiza vyuo vikuu vyote nchini kuacha mara moja urasimu katika kuwasajili wanafunzi wote ambao ni wanufaika wa Mikopo ya elimu ya juu
hayo yametolewa tarehe 9 novemba mjini Dodoma bungeni ambako waziri wwa elimu Prof.joyce Ndalichako ametolea ufafanuzi kutokana na kudaiwa kuwepo kwa ursimu mkubwa katika udahili wa wanafunzi wengi katika vyuo mbalimbali nchini
Naviagiza vyuo vyote nchini kuacha urasimu mara moja kuanzia sasa inasikitisha sana kuona baadhi ya vyuo vinaendelea kukwamisha juhudi za mheshimiwa raisi wetu wa awamu ya tano ya kuhakikisha wanafunzi wanapata stahiki zao kwa wakati unaotakiwa. Wizara yangu haitakifumbia maccho chuo chochote kiwe cha umma au binafsi kitachodiriki kukwamisha juhudi za mhe; raisi wetu wa awamu ya tano alafafanua Ndalichako
Pia serikali haitakuwa tayari kuona chuo chochote kinachokiuka maagizo ya serikali hivyo kitachukuliwa hatua kali za kisheria hata hivyo ameleza kuwa mkataba wa pesa hizo ni wa wa mwanafunzi na serikali na mwanafunzi kwani atalazimika kuziresha pindi akimaliza masomo yake hivo haoni umuhimu wa uwepo wa urasimu huo
kuna vyuo nimesikia vinawalazimisha wanafunzi kusoma programu ambazo hawajazichagua naagiza tume ya vyu vikuu TCU kuchunguza jambo hilo mara moja na kubaini kama kuna uwepo wa mambo hayo na kuchukua hatua kali pia kwa chuo chochote kinachofanya mambo hayo ya aibu kwa serikali makini ya awamu ya tano ambayo inaongozwa na Mh:John Pombe Magufuli.Ameongeza kuwa serikalil ipo makini sana katika swala hilo la kiutendaji amesema serikali inatarajia kufungua dirisha la rufaa kwa wanafaika wote wote ambao wamekosa mikopo katika awamu za awali na ambao wanaona mkopo huo bado hauja kidhi mahitaji yao ya kila siku kuanzia tarehe 13/11/2017 ili kuyapitia kwa uharaka zaidi na kuyatoa kabla ya tarehe 30 Novemba 2017
No comments:
Post a Comment